Sehem Ya 1; MJUE DR WILBERT KLERUU,Kifo Chake Na Muuwaji Kumfikisha Marehem Kituo Cha polisi Na Kujisalimisha

*Kifo Cha Dr Wilbert Kleruu Na Muuwaji Kumfikisha Marehem Kituo Cha polisi Na Kujisalimisha*

Dr Wilbert Kleruu alikuwa mzaliwa wa mkoa wa Kilimanjaro sehemu iitwayo Mamba (au Mwika), Moshi vijijini ambako siku hizi kunaitwa Vunjo. Alisomea uchumi wa kijamaa hadi ngazi ya PhD, na hasa alikuwa agricultural economist.

Alifanya kazi kwa karibu sana na Mwl Nyerere ambaye alimpenda sana, maana alimwona ni muumini wa siasa yake ya ujamaa na kujitegemea. Alijituma na kuiamini kwa moyo wake itikadi hiyo, kwamba ukombozi wa nchi utapatikana kwa mapinduzi ya kilimo cha kijamaa (ndio uanamapinduzi anaozungumziwa).

Alijitahidi pia kutekeleza itikadi hiyo kwa vitendo, na ndiyo iliyomgharimu maisha yake mwaka 1971 alipokuwa mkuu wa mkoa wa Iringa. Siku moja ya jumapili (hakuwa na jumapili huyu mjamaa) alikwenda kwenye shamba la mkulima mmoja aliyeitwa Saidi Mwamwindi, ambaye alikuwa na shamba kubwa sana, kwa lengo la kufuatilia maagizo yake aliyokuwa ametoa kuhusu shamba hilo, ndipo alipokorofishana na mkulima huyo maana yeye hakuzikubali hata kidogo hizo sera za kijamaa. Mwamwindi alikwenda nyumbani kwake akachukua gobore lake, akamfuata Dr Kleruu alipokuwa akampiga risasi na kumwua, kisha akapakia mwili wake kwenye Land Rover yake (pick up short chassis) na kupeleka kwenye kituo cha polisi ambako pia alijisalimisha.

Nyerere alihuzunishwa sana na kifo hicho, na hata kesi ya Saidi Mwamwindi ilipoisha na kupewa hukumu ya kifo, Nyerere hakusita kusaini, na ni mojawapo ya hukumu tatu tu za kifo zilizotekelezwa wakati wa utawala wa Mwl Nyerere.

Wengine wataongezea, lakini kama hapo ulipo unaweza kupata vitabu, tafuta kitabu kiitwacho "The Egalitarian Moment: Asia and Africa 1950-1980" kilichoandikwa na Donald Anthony Low (1995), habari hii ya Dr Kleruu iko kwenye ukurasa wa 52-53, kwenye chapter yenye heading "Richer Peasants and the State".

Unaweza pia kusoma journal article iliyoandikwa na Phillip Raikes mwaka 1979: Agrarian Crisis and Economical Liberalisation in Tanzania kwenye jarida la Journal of Modern African Studies Vol 17(no.2) pg 309-316, ambayo nimejaribu kukuwekea link yake hapa chini. Kifo cha Dr Kleruu kiliwahuzunisha watu wengi hasa wakulima wadogowadogo wa huko Iringa ambao walikuwa wakifurahia alivyokuwa ananyang'anya mashamba kwa wakulima wakubwa ili yalimwe kijamaa. Pia alikuwa ana tabia ya kuwafokea watumishi wa serikali hata wakurugenzi kwenye mikutano ya hadhara, pale alipoona sera zake za kijamaa hazijafuatwa kama alivyotaka, yaani alikuwa na ule ujamaa wa kibabe hasa uliokuwa Urusi (ajabu ni kwamba huyu alisomea Marekani!). Kwa namna fulani (ama kiasi kikubwa) alikuwa na 'ukali' kama ule wa Marehemu Sokoine. Raikes (1979) anaandika hivi kuhusu kifo cha Dr Kleruu kwenye rejea niliyotaja:

Post a Comment

0 Comments