Wilaya ya Ruangwa Yazindua Kampeni Chanjo ya Polio Awamu ya Tatu

Na Loveness Danielhttps://drive.google.com/uc?export=view&id=1tDUnpqjZjbyBWNgnL4-H8wOmOHePkXjG

Mkuu wa wilaya ya Ruangwa Mh.Hassan Ngoma amezindua rasmi zoezi la utoaji  chanjo ya   matone kwaajili ya kudhibiti ugonjwa wa kupooza (polio) leo tarehe 1 September 2022.

https://drive.google.com/uc?export=view&id=163U_IxM8JcIGrmu-SN57uo9taoj5qbdI

Utoaji wa chanjo ya matone ya polio katika Halimashauri ya Wilaya ya Ruangwa ni kampeni inayoendelea kwa awamu ya tatu ya utoaji chanjo hiyo muhimu inayotolewa nchini Kwa watoto wenye umri chini ya miaka 5  ambayo itafanyika Kwa siku 4 kuanzia tarehe 1 hadi tarehe 4 september mwaka huu 2022.

https://drive.google.com/uc?export=view&id=1150dAayzFdBlr5ESKcndpehG_dN758Dt

Aidha Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa imepokea dozi 22,240 ya chanjo ya polio ikiwa na lengo la kuwafikia walengwa 22,926.


Hata hivyo mganga mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Dkt.Salvio wikes  amewaomba wananchi kuendelea kupokea elimu zinapotolewa na wahudumu wa afya wanapofika kliniki pia kutoa ushirikiano wakati wa ufanyikaji wa huduma tembezi ya chanjo ya matone ya polio.

https://drive.google.com/uc?export=view&id=1OD5j2sMFd4joVNtO2lrgTWDkOLNhsSoe

Dkt.wikes amesema katika awamu ya pili ya utoaji chanjo ya polio Wilayani Ruangwa ilifanikiwa Kwa 117% ikiwa zaidi ya watoto 22,926 walipata chanjo huku Halmashauri ilikua na lengo la kuchanja watoto 19,654.


Mnamo tarehe 18Mei 2022 zoezi chanjo ya polio iliizinduliwa rasmi wilayani ruangwa na mkuu wa wilaya  Mh. Hassan Ngoma huku Halmashauri ikipokea chanjo dozi 24,160 na kusambazwa  kwenye vituo 40 vya kutolea huduma.


Polio ni ugonjwa wa kupooza Kwa watoto /ugonjwa wa kuambukiza wa mfumo mkuu wa Neva unaosababishwa na  virusi vinavyojulikana kitaalamu kama poliomyelitis.

Post a Comment

0 Comments