Msanii na mwanaharakati VITALIS MAEMBE,akamatwa na police

#1Yesterday at 10:23 PM
Leo wanafunzi wa chuo cha sanaa Bagamoyo(TASUBA), wameamua Kuandamana kupinga Chuo cha sanaa Kuajiri Walimu wasio na sifa, na uundwaji wa kozi bila kufuata utaratibu kwa lengo la kujipatia fedha unaofanywa na uongozi wa Chuo hicho. Kumbuka hiki ndo chuo pekee cha sanaa Tanzania nzima.
Katika harakati za kuzuia maandamano hayo, Polisi wamewakamata baadhi ya Wanafunzi kadhaa akiwemo Msanii wa Muziki wa Asili, Vitali Maembe. wapo mikononi mwa polisi wilaya ya Bagamoyo kwa tuhuma za kuhusishwa na sakata la kitaaluma kwenye Chuo cha Sana'a Bagamoyo.

Post a Comment

0 Comments