HISTORIA :Josiah Mwangi Kariuki, AFRIKA NA UAFRIKA VOL 1


Josiah Mwangi Kariuki, almaarufu kama J.M Kariuki. Mwanaharakati na mwanasiasa na maarufu, aliyekaa gerezani kama mwanachama wa Mau Mau, kundi ambalo lilikuwa limepigania uhuru wa Kenya mnamo 1963. Aliyechaguliwa kwenye bunge la Kenya na kuwa mtu muhimu kwa Rais wa Kenya. Mtu mwenye chachu ya maendeleo ambaye kukosoa kwake serikali hakukumpatia tunzo ndani ya serikali yamzee Kenyatta, bali maadui na kifo chake.

JM Kariuki alikuwa mtu mwenye utata toka alipozaliwa mnamo 1929 hadi mwaka aliyokutana na umauti 1975.

Inadaiwa ya kwamba, alikua mcheza kamari na alilelewa akiwa motto wa pekee wa kiume kwenye famiia ya watu watano.
Alilazimika kuacha shule kwa sababu ya kukosa ada na hapo ilimbidi aombe kazi kwenye shamba la wakoloni ili kupata pesa. Aliishi ki mkanda mkanda hadi hapo mwaka 1946 aliposhinda bet ya mashindano ya mbio za farasi huko Nakuru

Akatumia fedha yake ya bet kujiandikisha shuleni, kasha alijiunga na Mau Mau, na wakati Kenya ilipopata uhuru, aliingia rasmi kwenye ulingo wa siasa.

Hapo awali walikuwa marafiki wazuri na rais wa kwanza wa nchini Kenya bwana Jomo Kenyatta, wawili hao walikosa kuelewana baada ya JM kuhoji kuhusu wizi wa ardhi.

“Watu wetu waliokufa msituni walikufa wakiwa na udongo katika mikono yao huku wakiamini, wameanguka kwenye pambano kwaajili ya kurudisha ardhi yetu ... Lakini sasa zinachukuliwa na watu wachache ambao ni walafi na wabinafsi. Lazima tufanye kitu sasa, maswali kuhusu ardhi yatajibiwa kwa umwagaji damu. "

Haya yalikuwa maneno ambayo JM Kariuki aliyatamka wakati alipozungumza na kikundi cha wafuasi wake katika moja ya mkutano wake uliopigwa marufuku mnamo 1974 kama ilivyonukuliwa katika kitabu cha Simiyu Wandiba  2001 JM Kariuki.

Haikuchukua muda mrefu, ekari 700 za ngano kwenye ardhi ya Kenyatta huko Rongai zilichomwa moto na ng'ombe kuchinjwa vibaya. Huo ulikuwa mwanzo wa mwisho kwa JM.

Mara tu baada ya tukio hilo la kuchoma moto, ilisemekana JM Kariuki aliajiri vijana na kuwezesha kupata mafunzo ya wapiganaji wa msituni nchini Zambia. Chanzo cha uvumi huo pia kilidai kuwa kikundi hicho kilikuwa na mipango au kujihusisha na mabomu.

Februari 1975 mabomu mawili yaliyopandwa huko Nairobi, yalilipuka na mtuhumiwa number moja akawa JM. Kwasababu ya kutingwa na mawazo na matukio yaliyomtokea kipindi hiko, daktari alipendekeza bwana JM achukue mapumziko ya muda.



Alikuwa na rafiki wa kike anayeitwa Elizabeth Koinange. Kwa siri walikata tiketi ili wasafiri kuelekea Mombasa siku ya ijumaa usiku

Siku ilipofika, Daily Nation iliripoti kwamba rafiki yake alimwambia JM kwamba alifuatwa kwa siri na simu yake inafuatiliwa, kwa hivyo hafai kusafiri kwenda Mombasa. Wakaghairisha safari.
Dakika chache basi la OTC ambalo alipaswa alipaswa kusafiri nalo kutokea Nairobi lililipuka na kuwauwa abiria 27.

Nyakati za mwisho akiwa hai, alikuwa katika Hoteli ya Hilton, masaa 48 baadaye, alifuatana na walinzi wa Kenyatta, mnamo Machi 2, 1975. Inasemekana alikua na cheki ya dola 340 siku hiyo, pesa aliyokuwa ameikusanya.

Watu wasiojulikana kuwa ni majambazi au polisi waliingia hotelini na kumchukua JM moja kwa moja mpaka kwenye gari nyeupe na kamanda wa GSU Ben Gethi akishuhudia tukio hilo.Huku gari hilo likifuatwa na magari mengine manne.

Mwili wake ulipatikana kwenye barabara ya Ziwa Magadi, mwili wake ukiwa umechomwa. kifo chake kilipokelewa kwa hasira kubwa nchini Kenya. Mwili ulipelekwa mochwari ukiwa unatambulika kama mwili usiojulikana wa jambazi wa kijaluo.
Baadae mwili huo ulitambulika na mke wake ambaye alipewa taarifa na mtu asiyejulikana kuwa akautazame mwili wa mume wake mochwari.

Alijua mume wake hayupo nyumbani. Na alisisitiza kuwa mume wake alijua kuwa anafuatiliwa. Alipomshauri atembee na walinzi alimjibu “ hakuna wa kunizingua”

1 March Mrs Kairuki alimpeleka mume wake hospitali kwaajili ya maumivu ya mguu. Waliachana huko huko hospitali na Mrs Kairuki kurudi nyumbani.

Kabla JM hajapotea, aliacha ujumbe kwa wafanyakazi wenzake kuwa anatoka kuonana na Ben Gethi, jamaa wa usalama ambaye alimuita siku hiyo asubuhi.
Mke wa tatu wa JM alipoona mume wake haonekani, alitoa taarifa kwa familia nzima. Na kuamua kuuliza serikalini JM yupo wapi. Jibu walilopatiwa ni kwamba JM ameelekea Zambia mara moja.
Familia ilishtushwa na suala hilo kwakua passport yake ya kusafiria alikua ameiacha nyumbani. Ujumbe wa mwisho mke wake huyo ni ya kufika mjini Nairobi ili kuona mwili wa mume wake kipenzi.

Mke wake aliripoti kuwa. Sura ya mume wake ilibadilika na kuwa nyeusi, kana kwamba kuna kitu alimwagiwa usoni. Huku mguuni mwake akiwa ameandikwa mtu asiyetambulika. Ilimuuma kwakua alijua mume wake ni maarufu Kenya nzima.

12 March, afrisa wa polisi alithibitisha kuwa mwili wa Kariuki ulikuwa na majeraha mawili ya risasi.

Ripoti ya hospitali ilisema uso wa JM ulikua mweusi kama alivyoona mke wake kwasababu ya acid aliyomwagiwa ikiwa na dhumuni la kufanya asitambulike.

Wanafunzi wa Nairobi waliandamana kwakuona hali ya Kenya ni mbaya. Akiwa kama mwanasiasa na mwanaharakati wa tatu kuuawa ndani ya miaka 10.


Serikali iliruhusu uchunguzi kufanyika. Lakini kabla report haijatolewa, raisi Kenyatta aliamrisha baadhi ya majina yafutwe. Wengi walisema majina hayo alikua na ukaribu nayo.

Post a Comment

0 Comments