Download Jarida la Afrika na Uafrika, na HumphreyMoris/Twitreporter

TwitReporter/HumphreyMoris

 

Leo nimeona nisambaze Link ya mfano wa jarida ambalo nimekua nalitengeneza AFRIKA NA UAFRIKA na nimekua nikituma story kwa mfumo wa thread kwenye TL yangu. Kuna story chache kama 20 tu lakini kazi bado inaendelea. Na Huyu ni mimi na hii ni kama blurb.


Twitreporter jina kamili Humphrey Moris ni mtayarishaji, Mtangazaji na Mwandishi wa habari kutoka Tanzania. Huripoti matukio kupitia Mitandao ya kijamii na hasa mtandao wa twitter pamoja na blog yake binafsi.
Pia ni mwalimu wa mtandaoni ambae hufundisha masuala ya teknolojia kama vile (Matumizi ya kawaida ya kompyuta, Simu, Graphics designing:Picha na video ) Mtayarishaji wa video na vipindi mbalimbali vya televisheni, redio pamoja na Makala.
Mhitimu wa shahada ya mawasiliano ya umma na uandishi wa habari katika chuo kikuu cha mtakatifu Agustino Tanzania (SAUT) Mwaka 2019.


Nimekua nikijihusisha na uandishi wa habari wa mtandaoni kuanzia mwaka 2016 mpaka sasa. Na nimekua mpenzi sana wa masuala ya kijamii pamoja na historia kwa kipindi chote cha maisha yangu. Hii imenipelekea kuanzisha aina ya jarida lenye dhumuni la kuelezea matukio na historia mbalimbali kutoka barani afrika. Na kulipa jarida hilo jina la AFRIKA NA UAFRIKA

Jarida hili linarushwa mtandaoni bure kabisa. Document iliyotimia na kuwa na visa au matukio zaidi ya 10 huwekwa mtandaoni ili wapenzi wa jarida wapakue na kusoma kwa utulivu. Lakini pia matukio haya hutumwa kwenye akaunti yangu ya twitter (kwa siku habari moja). Nikiwa na lengo la kuwafanya watu wajitambue na kufungua minyororo ya utumwa wa kifikra kwa kushuhudia wengi na mengi bila kusahau yaliyofanywa mazuri na muhimu ili wote tuige au kuyaishi. Na pia ni sehemu ya chakula cha ubongo, kwamaana msomaji anaingiza kitu kipya kichwani mwake. Ninaweka mtandaoni nikiwa na dhumuni la kuyajadii pia yale ninayoyaandika na watu mbalimbali kwakua ni njia rahisi kupokea ushauri na maoni.
Sijawa na bajeti kubwa ambayo ingenisaidia kutembelea sehemu nyingi na kuandika yale ninayosimuliwa kwa kuona, kupiga picture na kutengeneza kitu kikubwa kilichojitosheleza zaidi ya hiki ninachokifanya. Kwa uwezo wangu mdogo ninakusanya taarifa zangu kupitia vitabu/simulizi na mitandao ya kijamii. Hakuna data hata moja mpaka sasa ambayo nimetumia mawazo yangu pekeangu.
Kazi ya kuunda jarida nimefanya kwa mikono yangu, picture nyingi ni za mtandaoni pamoja na taarifa baadhi.
SHUKRANI ZA DHATI kwa wote wanaofuatilia kazi zangu na kutosita kunishauri au kunikosoa. Pia kwa wote wanaonisaidia kusambaza ( mfano ku retweet) kwasababu sina uwezo wa kufikishia watu wengi taarifa hizi. Hivyo nategemea wasomaji wangu au watu wenye wafuasi wengi kuniinua,
Mkono wangu na ufundi wa kutengeneza jarida hili  ni zao imara la mwalimu wangu Elisha magolanga
Kichwa changu ni zao la vingi na mengi akiwemo mwalimu Richard Mabala, ni mtu wa kwanza ambaye ana jina kubwa kupenda nilichoandika mtandaoni na nnakumbuka siku hiyo alinifollow back japo sidhani kama anakumbuka.
Bila kusahau uandishi wangu ni zao kamili la Denis Mpagaze.
                    
JARIDA NI BURE
LAKINI KAMA UTAWEZA KUNICHANGIA KWENYE  HARAKATI ZANGU UNAWEZA NISAIDIA CHOCHOTE KUPITIA NAMBA ZANGU ZA SIMU
+255625773039 AU +255742965664.
NAPOKEA MAONI NA USHAURI, KIELIMU NI MTAALAMU WA MAWASILIANO YA UMMA HIVYO NINAWEZA WASILIANA NA MTU YOYOTE NA AKAFURAHI AU AKAPATA KITU ALICHOHITAJI KUTOKA KWANGU. NAPATIKANA MASAA 24


Post a Comment

0 Comments