HISTORIA & SHUJAA :,DEDAN KIMATHI, AFRIKA NA UAFRIKA VOL 1



Alizaliwa, akapambana na kuuliwa kikatili, tofauti na wengine, yeye hata nchi yake ilipanga kufutilia mbali historia yake na kumtambua. Marehem akumbukwe kwa mazuri bwana. Hata anapopumzika ajiskie kweli alifanya kitu. Hii ni imani yangu mimi muafrika, kama hyukubali pole sana.
Awamu mbili za utawala wa mwanzo wa Kenya baada ya uhuru, ile ya Mzee Jomo Kenyatta na baadaye wa mrithi wake, Daniel arap Moi, zilikataa kumtambua na kumpa Kimathi heshima ya kuwa mpiganiaji uhuru, zikimuangalia kama gaidi. Ndiomaana nikasema hata baada ya kifo chake walitaka kumpuuza.
Lakini baada ya uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi na kuingia madarakani kwa Rais Mwai Kibaki hapo mwaka 2006, serikali ilimtangaza Kimathi kuwa ni shujaa wa vita. Na mimi namuunga mkono Kibaki.
Alipofika umri wa miaka 15, alijiunga na shule ya msingi kijijini kwao, Karuna-ini, ambako alijifunza Kiingereza kwa ufasaha na kuitumia lugha hiyo baadaye kuandika mengi kabla na baada ya uasi wa Mau Mau. Alishiriki sana katika mijadala shuleni na alikuwa na kipaji cha kuandika mashairi. Mimi Kuanzia leo nampa jina la Dedan Makengeza.
Alijiunga na jeshi la uingereza lakini alifukuzwa kwa madai ya utovu wa nidham. Na hapo akaenda kwenye ualimu lakini alikosa kazi pia baada ya muda. Akagundua bado waafrika au Kenya haipo huru na kuingia rasmi msituni mwaka 1951 ambapo akajiunga na wapiganaji wa mau mau

Aliteuliwa kuwa katibu Mkuu wa wapiganaji hao katika tawi la Thomson Fall na kusimamia nidhamu kwa wanajeshi wa maumau. Inasemekana alisimamia viapo kwa wapiganaji hao na hata kutumia vitisho ili wanajeshi hao wakae kwenye mstari imara. Maana kwenye mapambano msaliti mmoja anaweza kusababisha matatizo kwa kikosi kizima. Hivyo Dedan aliwapika wapambanaji kisawasawa.
Mwaka wa 1951 alikamatwa na Wakoloni lakini askari weusi waliokuwa ndani ya kikosi cha usalama walimsaidia kutoroka.

Mwaka 1953, Kimathi akaunda Baraza la Ulinzi kuratibu shughuli za wapiganaji wote wa msituni.
Mwaka 1956, miaka minne tangu kuanza uasi huo, Kimathi alikamatwa katika misitu ya Nyeri na kundi lililoongozwa na Ian Henderson. Kukamatwa kwake kukawa mwisho wa vita vya msituni. Walikata mizizi mti wote ukaanguka lakini mapambano hayo yalikua chachu ya ukombozi na uhuru wa wakenya.

Alihukumiwa kifo na Jaji Mkuu O`Connor huku akiwa kitandani hospitali kuu mjini Nyeri. Alinyongwa mapema asubuhi ya tarehe 18 feb 1957 katika gereza kuu la Kimiti.
Mahala alipozikwa hadi leo hapajulikani.Juhudi nyingi zimefanyika ili kupata kaburi la Dedan. Kuna baadhi ya chapisho zilisema kaburi lake limepatikana lakini taarifa hiyo ilikanushwa.
 Kimathi anaangaliwa kama shujaa wa taifa na serikali ya sasa na kuna sanamu maalum la "Mpigania Uhuru Dedan Kimathi" katikati ya jiji la Nairobi, lililozinduliwa tarehe 11 Desemba 2006, katika kumbukumbu ya tarehe aliyouwawa.
“Siongozi magaidi. Ninaongoza Waafrika ambao wanataka serikali yao binafsi na ardhi. Mungu hakukusudia kwamba taifa moja litawaliwe na mwingine milele. “

Post a Comment

0 Comments