HISTORIA/SHUJAA :BIBI ZURA KARUMBI, AFRIKA NA UAFRIKA VOL 1

Mchawi mpatie mwanao amlee, kauli ina ukakasi hii. Ndio hatomuua, lakini je akimfundisha uchawi mtoto huyo na kuja kuwa balaa kwenye nyumba yako?. Kuna wachawi wameokoa watu na kupata tuzo. Wenzetu wa kabila Fulani wakikuhisi tu hata kama una macho mekundu wanakuua. Tumepoteza mashujaa wengi sana. Hii sio movie, maana usijedhania nataka kukusimulia hadithi za Merlin kwenye nchi ya Camelot. 

Huu ni mkasa wa kweli kuhusu bibi Zura Karuhimbi. Mwanamke aliyeweza kuokoa mamia ya watu katika mauaji ya kimbari nchini Rwanda 1994

Zura Karuhimbi hakuwa na silaha yeyote ya kujilinda wakati wanaume waliokuwa na silaha walipoizunguka nyumba yake na kumtaka awakabidhi watu aliokuwa amewahifadhi nyumbani mwake.
Mwanamke huyo alikuwa anajulikana kuwa na nguvu za giza.

Hali iliyowafanya kundi hilo la wauaji kuwa na uoga na kumfanya mwanamke huyo mzee kuwaokoa watu zaidi ya 100 kuwa salama wakati wa mauaji ya kimbari nchini Rwanda.

Vyumba viwili vidogo vilivyopo kijijini Musamo, kwa haraka vilikuwa sehemu salama kwa watusi, Waburundi na hata wazungu watatu walijificha humo wakati wa mauaji ya kimbari.

Makundi ya watu yaliripotiwa kuwa walikuwa wamejificha chini ya kitanda na eneo lingine la siri juu ya paa.

Huku wengine walisema kuwa alikuwa amewachimbia shimo kuwaficha.

Baadhi yao walikuwa watoto ambao walichukuliwa kutoka kwa mama zao waliokufa, alisema hivyo.

Karuhimbi alimwambia mwandishi wa habari wa Rwanda Jean Pierre Bucyensenge katika kumbukumbu ya miaka 20 ya mauaji ya kimbari kuwa ,

“Silaha pekee ya Zura ilikuwa ni kuwatisha wauaji kuwa atawaloga wao pamoja na familia zao, “ bwana Bucyensenge alieleza

Maisha yaliendelea huku akiwa ni mwanamke ambaye anaomboleza kupotea kwa mtoto wake katika vurugu hizo na binti yake ilijulikana kuwa aliwekewa sumu akafa.

Pamoja na umaarufu mkubwa alioupata kuwa alikuwa mchawi lakini hakuwa mchawi na wala hakuwahi kuwa mchawi.


Mwaka 2006, bibi huyo alitunukiwa tuzo ya kupambana na mauaji ya kimbari na rais wa Rwanda Paul Kagame, Tuzo ambayo alikua analala nayo kitandani siku zote . Tuzo hiyo ilimpa nafasi ya kusimulia namna alivyookoa watu wengine 50 katika miaka ya nyuma. Aliweza kumwokoa kijana wa kitutsi miaka ya 1950. Wahutu waliua watoto wa kiume wa kitutsi, bibi huyu alimsaidia mwanamke mmoja aliyebeba mtoto wa kiume kwa kumfunga shanga kichwani ili wauwaji hao wamdhanie ni motto wa kiume. 
Na ilimsaidia motto Yule kuokoka kwenye mikono ya wanyamera. Bibi Zura alimfananisha motto Yule na Rais wa Rwanda Paul Kagame. Na kusema, nimemsaidia Kagame ambaye leo hii amenipatia tuzo. Hii ikimaanisha bibi Yule alikua akiamini katika Karma ( wazungu wanasema goes around comes around) kitisho cha uchawi chaokoa mamia nchini Rwanda.

kama watakufa basi na mimi pia nitakufa, Hata kama ningejua mtuhumiwa yeyote , nisingeweza kumzuia.”



Post a Comment

0 Comments